Dogo Janja Akiri Ndoa Yake Imeupendezesha Muziki Wake Zaidi

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Dogo Janja amefunguka na kudai ndoa yake na staa wa Bongo movie IreneUwoya imezidi kupendezesha muziki wake anaofanya sasahivi.

Dogo Janja anafanya vizuri hivi sasa na wimbo wake mpya unaoitwa ‘Banana’ ambao umezidi kushika chati nyingi za juu Kwenye redio stesheni mbali mbali Lakini pia unashika namba moja YouTube.

download latest music    

Dogo Janja aliyefunga ndoa na Uwoya mapema mwaka jana amedai ndoa yake ndio imempa mzuka wa kuwa anafanya muziki mzuri zaidi kuanzia ngoma yake ya ‘Wayu wayu’ mpaka ‘Banana’.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Dogo Janja amefunguka haya kuhusu ngoma yake mpya na mchango wa ndoa yake:

 Kikubwa nimebadilika, naimba staili tofauti kabisa zikiwa na mchanganyiko wa ragga f’lan na hata kwenye ngoma yangu hii ya Banana utaona utofauti.

Kwa upande wangu ndoa imefanya muziki wangu kuwa muruaa, nina ndoa na muziki kama kawa ngoma zinatiririka tu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.