Dude Ashauri Wasanii Wapewe Elimu

Muigizaji wa Bongo movie Kulwa Kikumba maarufu kama Dude ameitaka serikali iwasidie elimu wasanii ili waweze kuelimika katika masuala ya uwekezaji.

Dude amedai mambo ya wasanii kupata matatizo au inapotokea wanaugua wanakosa pesa za kutibiwa mpaka kufikia hatua ya kuchangiwa pesa na serikali ni la Kutia Aibu badala yake wapate elimu ya uwekezaji.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Za Motomoto News Dude amesisitiza suala la wasanii kuugua na kushindwa kujilipia gharama za matibabu nje ya nchi limekuwa likimuumiza mno hivyo kuiomba Serikali kuwaboreshea mazingira ya kazi zao na kupatiwa elimu ya uwekezaji kwa hicho kidogo wanakichopata.

Tunaiomba Serikali ituboreshee mazingira ya kazi zetu maana tunateseka sana hasa pale tunapopatwa na magonjwa yanayohitaji matibabu ya nje ya nchi au hata hapa nchini. Pia tupate elimu ya uwekezaji kwa fedha hizi kidogo tunazopata maana hatuna elimu hiyo pamoja na bima ya afya”.

Siku chache zilizopita Msanii mkongwe wa Bongo movie Mzee Majuto alikosa kabisa pesa za matibabu mpaka kufikia hatua ya kuchangiwa na serikali ili akapate matibabu nchini India.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.