Emmanuel Mbasha Aburuzwa Mahakamani Baada Ya Kutelekeza Mtoto

Mwanamuziki wa nyimbo za injili ambaye pia alijizolea umaarufu baada ya kumuoa muimbaji wa nyimbo za Injili Florah Mbasha, ameburuzwa mahakamani baada ya Kutelekeza mtoto.

Habari za chini ya kapeti zinazoripotiwa na gazeti la Risasi Mchanganyiko, zinadai kuwa Mbasha ameburuzwa mahakama ya Kisutu na mwanadada Miriam Kawishe ambaye amedai amemtelekeza mtoto wao wa miaka mitatu aitwaye Avantica bila matunzo yoyote.

download latest music    

Unajua Mbasha naye ameburuzwa mahakamani kwa kesi ya kushindwa kutoa matunzo ya mtoto tangu alipozaliwa hadi sasa ana miaka mitatu na ilianza kutajwa wiki iliyopita huku ikitarajiwa kuendelea tena mwisho wa mwezi huu. Ninyi mtafuteni huyo mzazi mwenzake atawaeleza vizuri”. Kilisema chanzo cha habari.

Baada ya taarifa hizo , Risasi Mchanganyiko lilimtafuta mwanamama huyo aliyezaa na Mbasha, Miriam ambaye alikiri kwamba ni kweli, lakini hawezi kuzungumza sana kwani kwa sasa suala hilo liko mahakamani tayari pia ana wakili anayelisimamia.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.