Enock Bella Akiri Kufelishwa Kwa Kukosa Uongozi Wa Maana

Mwanamuziki wa Bongo fleva aliyejipatia umaarufu katika kundi la Yamoto Band Enock Bella amefunguka na kusema jambo pekee linalopelekea kusua sua Kwenye muziki ni kwa ajili ya kukosa uongozi wa maana.

Enock Bella amekuwa ndio msanii pekee kutoka katika kundi la Yamoto ambaye amekosa mafanikio kulinganisha na waaanii wenzake kama Aslay, Beka Flavor na Mbosso ambao wamepata mafanikio makubwa.

download latest music    

Bella anafunguka na kusema sababu pekee inayomfanya mpaka hivi sasa anasua sua hana ngoma za kutosha ni kukosa management ya maana ya kumsimamia ipasavyo.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Enock Bella amfunguka haya kuhusu suala hilo:

Mara nyingi kinachonifelisha kama Enock ni kuwa active katika kazi zake kwa sababu ya menejimenti ninazozipata mara nyingi huwa mbovu.

Yaani nafesli sana katika menejimenti lakini nikipata menejimenti inayojitambua nakujua muziki ni nini na dhamani ya msanii ipo wapi wanaweza wakashangaa Watanzania”.

Kauli hiyo imekuja mara baada ya kuachana na na menejimeti iliyokuwa inamsimamia kutoka nchini Burundi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.