Enock Bella Alitafuta ‘kiki’ Kwa Kudanganya Ameoa

Msanii wa Bongo fleva Enock Bella aliyepatia umaarufu kupitia katika kundi la Yamoto Band kutokana na kuwa na sauti nzito kabisa ametuhumiwa kwa kitendo chake cha kudanganya mashabiki zake ameoa na kusambaza picha za harusi mtandaoni ilimradi tu apate kiki.

Imekuwa ni jambo la kawaida sasa kwa wasanii wa Bongo fleva na Bongo movie kutengeneza kitu kinachoitwa ‘kiki’ ambacho kitu kinachotokea ni wasanii hawa hutengeneza skendo feki ambazo ni mbali na muziki wao na hivyo kuwavuta watu au mashabiki na kisha kutoa kazi zao ili zipate media attention. Wasanii hawa hutangaza ndoa feki, hudanganya kuwa ni wajawazito na hata hudanganya kuwa wana uhusiano na mastaa wenzao ilimradi tu watu wavutiwe.

download latest music    

Sasa msanii Enock Bella aliyesifika kwa kuimba kwa bezi alipokuwa Yamoto, ilidaiwa kuwa baada ya kundi hilo kuvunjika alitoa nyimbo ambayo haikufanya vizuri hivyo alimua kuwa atakapotoa nyimbo yake ya pili atengeneze kiki hiyo.

 

Alipohojiwa na kituo cha televisheni cha East Africa Enock Bella alifunguka yafuatayo kuhusiana na tuhuma hizo;

Unajua zile picha za harusi zilizo trend zilikuwa ni project tu ilibidi zitumike kwenye video ya Sauda lakini baadae zile picha zilitolewa kwa maana zisitumike tena maana director alisema tubadilishe kwa sababu wasanii wengi walishatumia harusi kwenye video zao ili kuleta utofauti ilikuwa lazima tutafute utofauti fulani kwaiyo baadaye zile picha zikawepo tu bila kazi kwaiyo watu wangu wa karibu wakanishauri zile picha tuziachie tu ili ziwe za kutafuta attention ya watu”.

Pia Enock Bella amekiri kuwa hajafunga ndoa bali zile picha zilitumika kwa ajili ya kutafutia kiki ili nyimbo yake ipae zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.