Enock Bella Amefungukia Tuhuma za Aslay Kuiba Daftari La Nyimbo za Yamoto Band

Aslay ni mmoja Kati ya wasanii anayefanya vizuri sana kwa hivi sasa mafanikio anayopata ni wasanii wachache wanaoweza kufikia ukitegemea kwa mtindo wake wa kutoa nyimbo kila baada ya muda mfupi.

Lakini mafanikio Kama haya lazima yaje na changamoto kadhaa kwa upande wa Aslay changamoto hiyo ni bendi yake ya zamani ya Yamoto Band iliyovunjika miezi michache iliyopita na kupelekea vijana waliokuwa wanaunda bendi hiyo kutengana.

download latest music    

Baada ya kuvunjika kwa bendi hiyo na Aslay kama solo artist, maneno maneno yalianza chini kwa chini ambapo moja kati ya habari zilizosambazwa na watu wasiojulikana na kushika kasi ya ajabu hivi sasa za kumchafua Aslay ni kuwa kitu pekee kinachompa Aslay mafanikio baada ya kuondoka Yamoto na kuwa na nyimbo nzuri kila siku ni kwa sababu wakati anaondoka Yamoto band aliiba daftari la nyimbo la Yamoto ambalo alishirikiana na wenzake kuandika.

Enock Bell ambaye alikuwa kwenye bendi ya Yamoto na Aslay amefungukia tuhuma hizo kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha  East Africa:

Unajua uzuri nchi yetu haijamkataza mtu kuongea kila mtu akijisikia kuongea anaongea chochote anachoweza kukifikiria lakini kiukweli ni kuwa Aslay bahati nzuri Mwenyezi Mungu kamjalia kitu chake cha kipekee ni msanii ambaye unaweza ukamwekea biti tu akafree style nyimbo nzima kwaiyo Ana uwezo wa kuandika nymbo hata nne kwa siku mbili anaweza kupangilia mashairi yake vizuri kwa muda mfupi na yakawa makali kwaiyo sio kweli kuwa aliiba daftari la Yamoto kwanza hatukuwa na daftari lolote”.

Enock alikataa tuhuma hizo na kudai kuwa sababu pekee watu wanasambaza habari hizo ni baada ya kuona Aslay anatoa nyimbo kali kila siku lakini amedai hicho ni kipaji chake tu na sio wizi.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.