Esha Buheti Afunguka na Kueleza Jinsi Mtoto Wake Alivyoiokoa Ndoa Yake

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Esha Buheti amefunguka na kuweka wazi jinsi mtoto wake wa mwisho aliyemzaa alivyoikoa ndoa yake.

Esha amedai mtoto wake aitwaye Claribel ameweza kwa asilimia kubwa kuiokoa ndoa yake ambayo alikuwa kabisa anaiona kama imeshavunjika na kukosa kabisa matumaini ya Kurudi tena.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Esha amesema kila akimuangalia mtoto wake huyo anakuwa na sababu nyingi za kumshukuru Mungu, kwa kuwa ndiye chachu ya kumfanya awepo kwenye ndoa yake mpaka leo.

Unajua kabla ya ujauzito wa mtoto wangu huyu ndoa yangu ilikuwa haina uhai kabisa yaani ilishikiliwa na uzi mdogo sana, lakini Mungu alipomleta mwanangu huyu na ndoa yangu ikarudi upya kabisa, nashukuru kwa hilo nina maelewano vizuri na mume wangu”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.