Esha: Jokate Usinichukie Mimi Ni Bendera Fuata Upepo

Muigizaji wa Bongo movie Esha Buheti ameendelea kumtolea povu zito mwanadada Jokate Mwegelo huku akimsihi asimchukie kisa Ali Kiba kuoa kwani yeye ni bendera fuata upepo tu.

Siku chache zilizopita Esha alimtuhumu Jokate kwa kumchukia kisa na mkasa alihudhuria harusi ya staa wa Bongo fleva Ali Kiba na mkewe Amina Mombasa nchini Kenya.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Esha amedai kuwa  amesikia kutoka kwa watu wake wa karibu kwamba mwanamitindo huyo anamchukia kwa sasa kutokana na kuwa karibu na Kiba kwenye harusi yake na mrembo Amina Khaleef.

Kama ni kweli Jokate atakuwa ananichukia kisa mpenzi wake wa zamani Kiba kuoa kama watu wanavyosema, basi atakuwa ananichukia bure“.

Lakini pia Esha ameweka wazi kuwa sio kosa lake kwani yeye ni kama bendera fuata upepo anafanya alichokuwa anaelekezwa kwani haikuwa harusi yake:

Mimi ni kama bendera tu nafuata upepo kwa hiyo wa kumchukia ni Kiba mwenyewe aliyeamua kumuacha yeye na kuoa mtu mwingine, na wala si yeyote yule ambaye yupo karibu na Kiba”.

Tangu Ali Kiba Afunge ndoa aliyekuwa mpenzi wake Jokate Mwegelo hajaposti kitu chochote Kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.