Familia Haitapewa Michango Ya Marehemu Masogange-Steve Nyerere

Muigizaji wa Bongo movie Steve Nyerere ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa kamati ya mazishi ya Agnes Masogange amesema pesa za rambi rambi zilizochangwa hazitapewa kwa familia.

Siku ya jana familia ya Masogange ililalamika kuwa hwajaona hata senti ya fedha ambayo wasanii wa Bongo movie waliochanga kwa ajili ya kumsomesha mtoto wa marehemu anayeitwa Sania.

download latest music    

Steve Nyerere amefungukia tuhuma hizo za kutokabidhi pesa hizo kwa ndugu wa Masogange na kusema kuwa pesa hizo haziwezi kukabidhiwa kwa familia.

Kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa Tv, Steve Nyerere amesema pesa hizo ambazo ni kiasi cha shilingi milioni mbili zimechangwa kwa ajili ya kumsaidia mtoto atakapoanza shule hapo mwakani.

Lakini pia Steve ameitaka familia ya Masogange iendelee kushukuru kwa mchango waliotoa kwa ajili ya kumzika ndugu yao na waache kuulizia Michango  ya pesa kwani sio ya kwao bali ni pesa za mtoto.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.