Familia Ya Agnes Masogange Yadai Haijapokea Michango Ya Marehemu

Familia ya marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ imelalamika kuwa haijapokea michango yoyote iliyokusanywa kipindi cha msiba wiki chache zilizopita.

Ndugu wa marehemu Agnes Masogange wakiwemo wifi zake ambao ndio wanaishi na mtoto mmoja wa Marehemu anayeitwa Sania wamesema hawajapata taarifa zozote juu ya fedha ambazo zilichangwa na Kamati ya wasanii kwa ajili ya malezi ya mtoto.

download latest music    

Kwenye mahojiano waliofanya na Planet Bongo ya East Africa Radio, mmoja wa ndugu hao aliyejitambulisha kwa jina la Sada, wamesema hawajapata taarifa zozote kutoka kwa kamati hiyo iliyoundwa na wasanii ambayo pia ilisimamia kwa kiasi kikubwa mazishi ya Agnes.

Toka tumekuja hatujapata taarifa yoyote bado hatujawasiiana nao mpaka dakika hii labda mpaka tuwatafute”.

Lakini pia familia hiyo imesema ina mpango wa kuendelea kumlea mtoto huyo kwani hata kipindi cha uhai wa mama yake  walikuwa wanamlea.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.