Familia Ya Diamond Imecharuka Baada Ya Zari Kuwapeleka Watoto Kanisani

Familia ya msanii wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz, inadaiwa kuja juu na kutofurahishwa na kitendo cha Zari kuwapeleka watoto wao kanisani.

Zari na Diamond waliachana mwezi uliopita lakini katika Mahusiano yao walifanikiwa kupata watoto wawili ambao ni Latiffah na Nillan ambao wanaishi na kama yao Africa ya kusini.

download latest music    

Habari zilizoifikia gazeti la Amani zimedai kuwa siku chache baada ya Zari kuonekana akiwapeleka watoto wake wote kanisani siku ya Jumapili kimewacharua familia ya Diamond ambao ni way mini wa dini ya kiislamu hivyo moja kwa moja wanataka watoto wao wafuate dini yao.

Gazeti la Amani linaripoti kuwa mwanafamilia mmoja  wa familia ya Diamond ambaye aliomba jina lake lisiandikee gazetini amesema kama familia wamekasirikishwa na suala hilo kwani walijua labda wataenda mara moja tu lakini imekuwa kila jumapili:

Awali Zari alipotupia picha ya kwanza ikionesha ameenda kanisani na watoto, tuliona labda ni maombi ya mara moja na pengine haiwezi kuwa tatizo lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda, tunaona amekomaa na kanisani sasa tunaona kama inaweza kuja kuwa tatizo hapo baadaye na watoto wakawa njia panda.

Si unajua wale watoto ni waislamu kwa sababu siku zote watoto huwa wanafuata kwa baba, sasa baadaye watakaporudi kwa Diamond na wakawa wameshazoea kwenda kanisani itakuwaje?” 

Baada ya kupewa taarifa hiyo gazeti hilo lili Fanta jitihada ya kumtafuta Diamond na Mama Diamond ambao wote hawakupatikana lakini walipomsaka Baba Diamond Abdul Juma aliweka wazi kuwa kama familia hawajafurahishwa na kitendo cha Zari kuwafundisha kuhusu mafundisho ya Kikristo pekee.

Hatukatai dini ni dini tu lakini kilichotushtua ni kwa nini tunaona anawapeleka upande mmoja tu.
Unajua hata kama yeye ameamua kurudi kwenye Ukristo lakini watoto anapaswa kuzungumza na mwenzake ili waamue pamoja”.

Baba Diamond alimalizia kwa kutoa msimamo mkali kuwa, kama familia watamsisitiza Diamond azungumze na mzazi mwenzake na waangalie uwezekano wa kuwapeleka watoto hao madrasa ili pia waifahamu dini ya baba yao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.