Familia Ya Diamond Yadaiwa Kugoma Kwenda Kwenye Birthday Ya Mtoto Wa Hamisa

Familia ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz imedaiwa kugoma kabisa kuhudhuria Birthday party ya mtoto wa Diamond aliyezaa na Hamisa Dylan.

Global Publishers wanaripoti kuwa Familia hiyo inadaiwa kususia mwaliko huo ambao ni wa Birthday ya Mtoto wa Mobetto na inadaiwa kuwa bize zaidi na maandalizi ya birthday ya Tiffah itakayofanyika South Africa.

download latest music    

Chanzo makini kilieleza kwamba familia ya Diamond imegomea kwenda kwenye bethidei inayoandaliwa na Mobeto kwa ajili ya Dylan ambaye pia ni mtoto wa mwanamuziki huyo inayotarajiwa kufanyika Agosti 7, mwaka huu.

Unaambiwa familia ya Diamond haitaki kusikia mtu anayeitwa Mobeto maana hawampendi hivyo licha ya kwamba Dylan amezaliwa mwezi mmoja na Tiffah lakini wao wako upande mmoja wa Tiffah“.

Kwenye mahojiano na Global Publishers Esma Platnumz ambaye ni dada wa Diamond amesema  kuwa hawezi kwenda kwenye birthday ya Dylan kwa sababu hawajawahi kualikwa kwenye sherehe zao hata siku moja, hivyo hawawezi kwenda wala hawatarajii kusogea.

Hivi ushawahi kuona klina Hamisa wanatualika kwenye ishu zao hata kidogo? Hivyo hatuwezi kwenda hata kidogo wala hatutarajii kabisa“.

Kumekuwa na maswali mengi juu ya birthday ya mtoto wa Hamisa na Diamond ambaye pia ana birthday hivi karibuni kwani  inayosikika ni  ya Tiffah na siyo Dylan ambaye pia ni mtoto wa Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.