Familia Yaingilia Kati Bifu La Zari Na Hamisa

Hakuna ubishi kuwa Zari adui yake mkubwa hivi sasa ni Hamisa hiyo ilianza tangu siku Hamisa alivyoanza kutembea na Diamond huku akijua wazi kuwa ni baba watoto wake.

Bifu hilo lilianza rasmi mwaka 2015 pale ambapo Zari alipata taarifa kuwa Hamisa anatembea na Diamond. Bifu lilipamba moto miezi miwili uliopita baada ya Zari kugundua kuwa Diamond amezaa na Hamisa na hapo walianza kurushiana vijembe mtandaoni

download latest music    

Zari na Hamisa wamedaiwa kuwekwa kitimoto ili waache kurushiana vijembe kwenye mitandao ya kijamii, gazeti la Risasi limeelezwa kwa nyakati tofauti kila mmoja aliwekwa kitimoto na ndugu wa msanii wa mzazi mwenzao na kutakiwa waache malumbano hayo mtandaoni kwani hayaleti picha nzuri kwao ukizingatia kosa limeshafanyika na amekiri hadharani.

Walichoelezwa ni kwamba tu waache kutupiana vijembe mtandaoni kwani wao hivi sasa hata kama hawata kuwa wake wenza lakini tayari Diamond ana damu yake kwa Hamisa, ameshakiri aliteleza na kujikuta kwenye uhusiano naye hadi kufikia hatua ya kuzaa naye. Mtoto ameshazaliwa na ni damu ya msanii na mwisho wa siku atalazimika kumpa mahitaji yake kama mwanaye hata kama hataendeleza mahusiano na mwanaye”.

Chanzo hiko ambacho ni mwana familia wa karibu aliendelea kutiririka kuwa sasa hivi wanashukuru Mungu, kwani warembo hao wawili kila mmoja kwa wakati wake ameelewa somo na hivyo kuacha kurushiana maneno maneno kwenye mitandao ya kijamii maana zamani ilikuwa haipiti siku mbili bila kutibuana mitandaoni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.