Ferooz Ataja Sababu Zilizopelekea Ukimya Kwenye Muziki

Msanii mkongwe wa Bongo fleva Ferooz aliyewahi kutengeneza hits kama Starehe, Barua na Bosi na myinginezo amefunguka na kuongelea ukimya wake Kwenye gemu ya Bongo fleva.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Ferooz amefunguka na kuweka wazi kuwa pamoja na miaka mingi kupita bila kusikika lakini bado anapambana na gemu na mwili kukata tamaa:

download latest music    

Nipo napambana maana game ya muziki ni kama maisha mengine ambayo ni mzunguko unaweza ukawa juu au ukashuka. Napambana kupanda juu upya kwani Sijaachana na muziki na siwezi kwa sababu muziki ndio maisha yangu ila ni changamoto tu zilinipitia ndio maana nikawa kimya”.

Lakini pia Ferooz amefunguka na kukataa tetesi za k amna kundi lao la Daz Nundaz lilivurugika kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya:

Hapana hatukujiingiza kwenye madawa ya kulevya kwa sababu kuna vitu ambavyo vinatokea kwenye kundi kama migogoro mara huyu anasema hivi, mara vile nikaamua kuhama kwenye menejimenti kuna kipindi nilikuwa kwa Mkubwa Fela, unajua mkishaanza migogoro lazima mshuke kwenye kazi mkiwa kundi na kikubwa ni kwenye mgawanyo wa fedha ndio ilikuwa shida na si kweli kwamba madawa ya kulevya ndio yaliua kundi ni maneno tu ya watu wakiona unashuka wanazungumza yao lakini mimi nipo safi ukiniangalia na hata sauti yangu pia iko safi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.