Fid Q Aanza Kazi Rasmi TUMA kwa Kuwasilisha Maombi Serikalini.

Msanii wa muziki wa hip-hop nchini Fared Kubanda maarufu kama Fid q ameanz akazi rasmi kwa kutuma maombi kwa serikali kuwasaidia wasanii kutatua matatizo yao ya kimaslahi kwa kuwa wao hawana sehemu yoyote ambayo wanaweza wakalalamika kuhusu matatzo wanayoyapata wakiwa kazini.

Kwa kuitumia siku ya wafanyakazi, Fid  Q ambae siku moja iliyopita alitoka kuchaguliwa  kuwa mwenyekiti wa uchumi na fedha katika chama cha wasanii wa kizazi kipya Tanzania.

download latest music    

Sanaa ni sekta rasmi sasa hivi lakini bado haijatungiwa sera , hivyo ni sawa na kuwa na ofisi isiyokuwa na kanuni, taratibu wala sheria kwa kifupi  bado tunaongozwa na sera ya utamaduni .tunayofura kubwa kwa kutumia siku hii ya wafanyakazi kwa kuikumbusha WIZARA na serikali kwa ujumla kutuundia  sera ili sanaa yetu iweze kuleta tija kwa serikali.

Kwa kuongezea Fid Q anasema kuwa wasanii wamekuwa wakilipa kodi kubwa kwa ajili ya kazi zao lakini kazi zao hazilindwi hivyo hii inahatarisha  uchumi wa wasanii kwa sababu itafika sehemu watakuwa hawana faida wanayoipata kutoka katika kazi zao.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.