Fid Q Akanusha Kuwa na Bifu na Joh Makini
Msanii wa hip hop nchini kwa muda mrefu Fid q amefunguka na kusema kuwa hana bifu lolote na msanii mwenzake joh makini kama ambavyo imekuwa ikisemekana katika mitandao ya kijamii kuhusu wao kuwa na bifu hasa baada ya kutoa wimbo wake mpya ambao kuna baadhi ya maneno yalionekana kumlenga msanii huyo.
Alipokuwa akiongea na Big Chawa kutoka planet bongo ya EATV , Fid q anasema kuwa kutokana na kuwepo na maneno katika mitandao ya kijamii kuhusu kuwepo kwa bifu kati yao ndio maana aliamua kumuimbia msanii huyo.
La hasha wimbo wangu wa kibiriti hauna uhusiano owowte na joh makini kwa lolote bali ni wimbo ambao unanihusu mimi kwa 100% , kwa sababu ninaongelea wale watu waliokuwa wakiniponda kila ninapotoa kazi zangu, kwaio nimejilenga mwenyewe na wala sijatoa kwa ajili ya mtu yoyote.
Hata hivyo pia joh makini alisema kuwa atatoa wimbo kwa ajili ya msanii Fid q kwa sababu ya sikukuu yake ya kuzaliwa.