Fid Q Akerwa na BASATA, Asema huko ni kukomoana.

Msanii mkongwe wa bongo fleva Fid Q, ameshangazwa na uamuzi wa BASATA kwa kumfungia msanii Roma miezi sita ilhali muziki ndio kitu kikubwa anachokitegemea katika maisha yake ya kila siku.kupiti aukurasa wake wa Twitter Fid Q aliosema kuwa BASATA wamekuwa wakifanya hayo yote kama kuwakomoa wasanii lakini sio kuwarekebisha.

Kwa kuendelea kuonyeshwa kukerwa kwake , Fid Q alisema kuwa kufungiwa kwa nyimbo hizo kutokuchezwa katika vituo vya radio na tv ilikuwa ni adhabu tosha kabisa kwa msanii huyo lakini sio kumfungia kabisa.

download latest music    

Maneno ya Fid q yalikuja baada ya msanii wa hip-hop Roma Mkatoliki kufungiwa kufanya kazi zake za sanaa kwa mizi sita baada ya kukahidi agizo la kubadilisha baadhi ya maneno.

Na hili swala la kumfungia msanii asifany kazi kwa muda wa miezi sita kisa tu kwenye muziki wake kuna neno moja au kumi  yeney ukakasi sio sahihi…kuzizuia zisichezwe kwenye radio au tv ilikuwa ni adhabu tosha kabisa.@basatatanzania hii tabia ya KUKOMOANA mmeitoa wapi.H

Hata hivyo baada ya kuandika hivyo basata walikuja kumjibu na kumwambia kuwa lengo lao kubwa ni kuwarekebisha wasanii na sio vinginevyo

Ndugu @Fid Q wewe binafsi hujawahi pata tatizo kama hili,tungo zenye maadili na zisizo na matusi hujenga jamii yenye afya.tukumbushane,tusimamiane, na kufanya sanaa safi.Fuatilia tamko la Naibu Waziri aliyomfungia Roma leo na kumpa onyo Nay wa Mitego.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.