Fid q Apokea Tuzo ya Heshima , Wana Mwanza Wamshukuru kwa Kuwawakilisha Vizuri katika Muziki.
Rapa na Staa wa muziki kutoka Tanzania, Fareed Kubanda a.k.a Fid Q amepokea tuzo ya heshima ya kuwakilisha vyema kanda ya Ziwa kupitia Muziki toka kwa wataalam wa masuala ya mazingira Tanzania ‘KIJANI CONSULT TZ’.
Kupitia Ukurasa wake rasmi wa Instagram, Rapa Fid Q aliweka Picha za mwanae wa kwanza wa Kiume, ‘Feisal’ akiwa kakaa kando ya Tuzo hiyo na kuandika:
“Jana nimepokea TUZO YA HESHIMA YA KUIWAKILISHA VYEMA KANDA YA ZIWA KUPITIA MZIKI toka kwa wataalam wa masuala ya mazingira waitwao KIJANI CONSULT TZ… MWANZA ninakuja na team nzima ya SPORTS MUSIC ili tusherehekee TUZO hii pale UWANJA WA KIRUMBA leo kuanzia mchana hadi mida mibovu.. karibuni sana “.