Flaviana Matata Awatolea Uvivu Wenye Mapenzi ya Kinafiki Kwa Watu Waliokwisha Kufa
Imekuwa ni kama tabia siku hizi kwa baadhi ya watu kuonyesha kuwajali , kuwapenda na kuwakumbuka watu ambao walikwisha kufa wakati kipindi watu hao wakiwa hai walikuwa hawana hata muda wa kuwaonyesha kuwa wanawapenda.
Flaviana Matata ameguswa na swala hilo na hajanyamaza kuhusu swala hilo hivyo kaamua kuwatolea uvivu na kuonyesha kuwa tabia hiyo inakera na kuwaambia kuwa watu wakishakufa ndo wanaanza kuwaonyesha kuwa walikuwa wakiwajali wakati walikuwa na muda wa kuwajali hata kabla hawajafa.
mapenzi tunayowapa au kuwaonyesha watu katika page zao wakiwa wameshatutoka ebu tujaribu kuyaonyesha wakiwa wakiwa hai bado itapendeza zaidi #justthinkoutloud