Flora Mbasha na mumewe wa zamani wakorofishana tena

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Flora Mbasha na Emmanuel Mbasha waliachana miaka mitatu zilizopita lakini bado wako wakorofishana kwenye mtandao.

Emmanuel amemtupia maneno mke wake wa zamani baada ya kuzuka uvumi kuwa Flora alichapisha kitabu chake kinachoitwa ‘Siri za Flora Mbasha’ ambacho kinazungumia vitu mbaya kuhusu Emmanuel Mbasha.

download latest music    
Flora Mbasha na Emmanuel Mbasha

Ijumaa Wikienda lilimtafuta Emmanuel ambaye alionekana kuwa mwenye hasira kali alipoulizwa kuhusu kitabu cha mke wake wa zamani.

“Sipendi ujinga kwani watu hawawezi kuuza hicho kidaftari chao mpaka watafute kiki kwangu? Mbona wengine wanauza vyao kwa utaratibu mzuri? Mimi ninaingiaje kwenye ishu za huyo Flora? Zaidi ya miaka mitatu sipo naye na ni mke wa mtu, ninamuomba atulie na akome kunitajataja,” Emmanuel Mbasha alisema.

Kwa upande wa Flora alipotafutwa kuhusu ishu ya kumchafulia jina mume wake wa zamani, alisisitiza kuwa habari hizo za mtandaoni hazikuwa za kweli isipokuwa ni kweli kitabu chake hicho kimeshatoka na kinaelezea kiundani mambo aliyoyapitia kwenye ndoa yake na Mbasha kabla ya kuolewa na David Kusekwa.

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere