Florah Afunguka Baada Ya H.Baba Kukiri Kumiss Uwoya

Msanii wa filamu za Bongo movie, Florah Mvungj amefunguka Baada ya mume Wake ambaye ni Msanii wa Bongo fleva H. Baba kukiri kumiss Ex Wake Irene Uwoya.

Siku chache zilizopita H-Baba kupitia  ukurasa wake wa Instagram aliweka picha ya Irene Uwoya kisha kuandika kuwa amemmisi, jambo lililowashangaza wengi kwani siku za nyuma kidogo aliwahi kumponda na kusema haoni ndani kwa mke Wake Flora.

download latest music    

 

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Florah Mvungi amedai haoni tatizo kwa Mume Wake kumkumbuka Aliyekuwa Mpenzi Wake isitoshe amedai yeye hana wivu.

Watu wanakuza mambo sana, mbona ni hali ya kawaida sana, ni kumbukumbu tu ambazo mtu zinamrudia, anafanya anachojisikia, ameona ni vyema kushea kumbukumbu zake na watu kwenye mitandao, sijaona shida yoyote na wala sijahisi wivu“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.