G-Nako Aongelea Nyimbo Yake Kufananishwa Na Ya Nikki Wa Pili

Msanii wa bongo fleva G-Nako kutoka kundi la Weusi ambalo linafanya vizuri katika muziki amefunguka na kuongelea tuhuma juu yake kuhusu nyimbo yake ya Energy  kufananishwa na ile ya msanii mwenzie kutoka katika kundi hilo hilo la Weusi Nikki wa Pili unaojulikana kama Quality Time.

Katika ngoma iyo ya quality time ambayo ambayo g-nako amemshirikishwa na  nikki wa pili pia, inaelezea jinsi  mtu anavyokuwa ameteseka na maisha ya msoto kwa muda mrefu lakini sasa hivi anakula good time baada ya kustrugle,lakini kama wimbo wa energy wa G-Nako anaelezea jinsi anavyotaka kuwa na good-times bila kuletewa vikwazo,  baadhi ya mashabiki wamekuwa wakisema kuwa ukisikiliza nyimbo izi kuna baadhi ya idea zinafanana hivyo wanataka kujua nani kam-copy mwenzake, hivyo G-Nako kaongea kuhusu tetesi hizo.

download latest music    

Wanaposema Energy inafanana na Quality time sijajua wanataka kuifananisha upande upi,kwa sababu ukiangalia aina ya uandishi na mdundo uliotumika pia ni tofauti kabisa,ukisikiliza energy kuna radha flani ya Afro Pop wakati  pia nimeimba rumba kama sio rumba,lakini katika Quality time kuna  kama Pop,mada niliyozungumza kwenye energy ni tofauti kabisa ni ile ya quality time ambapo nikki alikuwa akizungumzia muda wake mzuri yeye kama yeye kwamba unapenda kufanya nini katika muda wake mzuri lakini energy inazungumzia jinsi ya kuondoa bad energy, na giza karibu yako na kuwa karibu na watu wanakupa ile good energy sasa “ alifunguka G-Nako

Hata hivyo G-Nako  ambae wapo katika kundi moja na Nikki wa Pilli anawahakikishia mashabiki kuwa kazi zao zote kabla hazijatoa huwa wanasikiliza kwanza wote , ivyo ufanano wa kazi hauwezi kutokea kabisa na mara nyingi uwa inatokea kazi zikafanana au kujirudia  huwa wanafuta na kurekebisha kabla ya kutoa”kabla kazi yoyote haijatoka huwa tunakaa wote na tunasikiliza ,hivyo swala la kufananisha kazi hii na kazi hii ni  kitu hakiwezi kutokea kabisa, na mara nyingi ikitokea tunarekebisha” alimalizia G-Nako.

G-Nako na Nikki wa Pili wote wanaunda kundi la Weusi akiongezea msanii mwenzao Joh Makini, Weusi ni moja ya kundi linalofanya vizuri sana katika muziki wa tanzania wakifanya kazi mmoja mmoja na wakifanya kazi kama kundi.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.