Gabo: Bongo Movie Wameacha Kazi

Muigizaji kutoka tasnia ya Bongo movie Gabo ameibuka na kudai kuwa wasanii wenzake wa Bongo movie wameacha kazi.

Kiukweli kwa mwaka huu tumeshuhudia jinsi Bongo movie ilivyoporomopa ingawa hatua za kufa kwa Bongo movie hazijaanza sasahivi lakini huu mwaka umeshinfilia kabisa like kinachosemwa kila siku kuwa tangu Kanumba amekufa Bongo movie nayo imekufa.

download latest music    

Mwaka huu mzima vipaji vya wasanii wengi wa Bongo movie zimeelekezwa kusiko sanaa kwani kuna mambo mengi yamefunika sanaa ikiwemo skendo za mahusiano kwa wasanii wengi, suala la siasa ndio kabisaa limepoteza wengi na pia skendo zimekuwa nyingi kuliko kazi.

Gabo ni moja kati ya wasanii wa Bongo movie anayefanya vizuri kwenye tasnia hii lakini pia amekiri kuwa wasanii wengi wa Bongo movie wamesahau kazi yao ya kuigiza lakini wameingia na kufanya kazi za watu wengine ambazo ni mbali kabisa na uigizaji wa filamu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na East Africa katika kipindi cha Enews amefunguka haya kuhusiana na ishu hiyo:

Ningezungumza kimapana zaidi ingawa najua ikawa inawagusa baadhi ya watu lakini wasisikitike lakini wachukue kama namna ya kujifunza wengi wetu tumeacha kazi zetu na kufanya kazi za watu wengine hivyo imepelekea kazi zetu kuharibika kuacha kazi yako kufanya kazi za wenzako unachanganya mashabiki ninachopenf kuwashauri wasanii wendaangu ni kuwa tubaki kufanya kazi zinazotuhusu na hii itatusaidia kukuza zaidi Industry yetu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.