Gabo Hana Hadhi ya Kuwa na Bifu Na Mimi- Duma

Muigizaji wa Bongo movie Daudi Michael maarufu kwa Jina la usanii kama Duma amefunguka na kudai kuwa hana bifu na msanii mwenzake Gabo na wala hana hadhi hiyo.

Kwa muda mrefu kumekuwa na kama ugomvi fulani kati ya Duma na Gabo na hata juzi juzi tu wawili hao wameonekana wakirushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii na hata vyombo vya habari.

download latest music    

Lakini Duma amedai hana bifu na Gabo na taarifa zinazoendelea kusambaa Kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii sio za kweli.

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani, Duma alisema hayupo katika bifu na Gabo kama watu wa mitandao wanavyovumisha ingawa hana mawasiliano naye kwa sababu hana kitu cha kuongea naye ila akiwa na kazi anaweza kufanya naye na akamlipa.

Sina bifu naye kabisa na wala hatuna mawasiliano kwa sababu mimi ni bosi wa kampuni yeye ni msanii wa kuigiza sasa tutaongea kuhusu nini? Labda nikiwa na kazi nitamwita afanye na nitamlipa ila najua yeye hawezi kuniita kwa sababu hajawahi kuzalisha filamu”.

Kwa muda mrefu sasa wasanii hawa wamekuwa wakisikika wakirushiana madongo kama hayo lakini sababu kamili ya kutoelewana haijulikani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.