Gabo na Duma Watoleana Maneno Kisa Kauli Ya ‘Kanumba Wapya’

Staa wa Bongo movie aliyejishindia tuzo ya msanii bora wa kiume Gabo amejikuta katika vita ya maneno a Msanii mwenzake Duma baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu Marehemu Steven Kanumba.

Gabo alipofanya Interview na kituo kimoja cha habari, Gabo alisema ili kuiokoa Bongo Movie wanahitajika kuandaliwa wakina Kanumba wengine watakaoweza kuikoa tasnia hiyo.

download latest music    

Baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa Gabo, Duma amemjia juu na kusema hajapendezwa na kauli hiyo kwani yeye na wasanii wenzake wana uwezo sana na watu waache kumtaja Steven Kanumba.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Duma alimwaga povu hili:

Kama kweli wewe unajiamini ni msanii mzuri Ian uwezo unapambana na unajituma huwezi ukasema tunahiyaji kanumba wengine kwani sisi hataweza kufanya alichofanya Kanumba? TUnaweza ila cha muhimu ni kujituma na kujua wapi tunapokosea.

Lakini pia Duma aliendelea kumtolea povu zito Gabo ikiwemo kumtolea maneno makali:

Unajua sio kila staa ana akili timamu kuna wengine mitambo tu tupo nao Kwenye Industry lakini ndio uwezo wao umeishia hapo lakini kama unajiamini uwezo wako unaweza kufanya kazi kubwa zaidi”.

Lakini pia Duma amewataka watu waache kumtaja taja Marehemu Kanumba lakini badala yake waelekeze juhudi zao Kwenye kupiga kazi nzuri zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.