Gigy Money Adai Yeye na Ali Kiba Wako Level Moja

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money amefunguka na kudai yeye kama ilivyo kwa Msanii mwenzake Ali Kiba wanaweza kuhit na nyimbo moja kwa mwaka mzima.

Gigy Money amefunguka na kudai hapendi kutoa nyimbo back to back kama wasanii wengine kwani inaweza kuua brand yake bali hupendelea kutoa nyimbo mara moja moja.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa East Africa amefunguka haya:

Siku si nyingi nakaribia kuachia kazi yangu mpya, watu wakae tayari naamini wimbo wangu utatingisha kinoma. Sipendi kutoa ngoma mpya mfululizo kwasababu huwa napenda kujikuta Alikiba kidogo, maana ninaweza ku-hit bila ya kutoa ngoma mwaka mzima”.

Lakini pia Gigy Money Anna mtazamo tofauti na wasanii wenzake pale linapokuja suala la kutoa Albamu kwani amedai hana mpango huo:

Sio kila msanii atakuwa na ubavu wa kuingia studio na kurekodi nyimbo 10 ili atengeneze albamu, kwangu mimi watu watasubiri sana katika hilo ila kama watu wanataka kuni-enjoy basi waendelee kunisikiliza kwenye ‘single’ moja moja, kwa maana sina hiyo pesa ya kutengeneza albamu kiukweli, halafu siwezi kujifungia studio muda wote kufanya kazi wakati mwanangu ananitegemea”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.