Gigy Money Asema Hamjui Wema Sepetu
Mwanadada Gigy Money ambae hakosi kuwa na drama kila siku anasema kuwa hamjui mwana dada Wema Sepetu na kwamba yeye ndie msani pekee wa kike ambae anafanya vizuri kwa sasa kuliko msanii mwingine yoyote hapa bongo .
Akiongea kwa kujiamini gigy money anasema kuwa kutokana na madili anayoyapata sasa hivi yanayomuingizia hela hakuna msanii wa kike wa kumlinganisha nae wa sasa.
Swala la gigy money kuwa akisema hawajui baadhi ya mastaa hapa bongo liekuwa la kawaida kwake kutokana na kuwa na tabia ya kusema hivyo mara kwa mara kwa baadhi ya mastaa wakubwa .
Gigy money ambae baada ya kujifungua alianza kufanya kazi na kusaini mikataba mbalimbali ya kumuingizia pesa ansema kwa sasa hakuna msanii wa kike bongo anaemfikia.