Gigy Money-Nilitembea na Ali Kiba Pamoja na Abdu Kiba

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money ametoa kali baada ya kukiri kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Staa wa Bongo fleva Ali Kiba pamoja na mdogo wake Abdu Kiba.

Gigy Money ameweka wazi kuwa ametembea na ndugu hao wawili lakini sio kwa wakati mmoja bali ilikuwa ni nyakati tofauti maana alikutana nao tofauti tofauti.

download latest music    

Gigy Money alifunguka hayo Kwenye Interview yake na kipindi cha Kikaangoni cha East Africa Tv ambapo alikiri kuwa wakati anaanza Mahusiano nao hakujua kuwa walikuwa ni ndugu:

 Kweli nilitembea nao mbona kawaida kwani nilikutana nao muda mmoja? Kwanza nilivyotembea nao sikuwa najua kama ndugu.

Halafu isitoshe mimi sina makosa mwenye makosa ni Ali Kiba kwani alijua natembea na mdogo bado akanitaka”.

Gigy Money ameanika kuwa Mahusiano Yake na Ali Kiba na Abdu Kiba yalikuwa siku nyingi kabla hajaanza kuwa video vixen ambapo enzi hizo alikuwa anakutana na wasanii club ambapo alikuwa anapenda kutembea na wasanii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.