H.Baba- Wasanii Wanaishi Maisha Ya Uongo Ya Kuigiza Wana Pesa

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva aliyewahi kutamba miaka ya nyuma na kibao chake cha mpenzi bubu, H.Baba amewachana wasanii wenzake na kusema wanaishi maisha ya uongo.

H. Baba amedai kuwa wasanii wengi sana wanatumia mitandao ya kijamii kufanganya mashabiki kwa pesa za kuazima kwa watu ili tu kuwaaminisha wako vizuri lakini kumbe kiukweli wanaishi maisha magumu sana.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, H. Baba ametoa povu hilo zito kabisa dhidi ya Wasanii Wenzake ingawa hakutaja majina:

Wasanii wanaishi maisha ya uongo, anapost picha ana pesa kumbe ameomba kwa jirani apige nazo picha tu lakini ukija kuangalia maisha yake unakuta maisha yake ni magumu sana“.

Hii sio mara ya kwanza kwa wasanii kunyoosheana vidole kuwa wanaigiza maisha kwa watu lakini kiuhalisia hali zao ni mbaya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.