Hakuna Bifu Kati Ya Ali Kiba na Diamond- Sallam Sk

Meneja wa Staa wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz, Sallam Sk amefunguka na kuweka wazi kuwa hakuna bifu kati ya Diamond na Ali Kiba.

Sallam amedai kuwa viongozi wa WCB wanakutana mara kwa mara na uongozi wa Alikiba na kuzungumza mambo mbalimbali.

download latest music    

Kwa muda mrefu kumekuwa na tetesi za kuwepo kwa bifu kati ya Diamond na Ali Kiba ingawa kila mmoja amekuwa akikataa na kusisitiza kuwa hakuna bifu.

Kwenye mahojiano na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Sallam alifunguka mambo mengi huku WCB pamoja na muziki ambapo pia alifunguka kueleza kwamba sio kweli kwamba Diamond ana bifu na Alikiba huku akienda mbali zaidi kwa kudai viongozi wa label hizo mbili hukutana mara kwa mara.

Kati ya Ali na Diamond hakunaga bifu, na haijawi kutokea, na uongozi wa Alikiba na WCB huwa unakutana mara kwa mara kuzungumza,” alisema Sallam. “Bifu ilitengenezwa na sisi baada ya kuona watu wanapenda hivyo vitu tukavitumia kwaajili ya kupromote wimbo wetu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.