“Hakuna Mwanamke Aliyeniliza Kama Wema”- Diamond

Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz anazidi kutengeneza headlines kwenye mitandao ya kijamii Ikiwa albamu yake ya ‘A boy From Tandale’ Ikiwa sokoni kwa hivi sasa.

Diamond amefunguka na kueleza ya moyoni mwake ambapo amekiri kuwa hakuna mwanamke ambaye alikuwa kumliza kwenye mapenzi kama Wema.

download latest music    

Diamond amefunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya nchini Kenya na Citizen Radio na Willy .M. Tuva, ambapo amedai Wema ni mwanamke ambaye alimtambulisha sana machozi.

Mara ya mwisho kulia kwa sababu ya mapenzi ni nilivyokuwa na uhusiano na Wema Sepetu dah yule mwanamke ameniliza sana hadi nakumbuka kuna siku nilikuwa pale home nipo gym babu Tale akawa ameona kuna maambo mabaya mabaya mtandaoni akaniambia mdogo wangu si uachane naye? Mi nakumbuka nikamwambia yaani sikudanyi bosi yule mwanamke nikiwa naye najisikia kama niko peponi  kwaiyo hata tulivoachana alikuwa haamini”.

Lakini pia Diamond amesisitiza kuwa ni kweli amemwaga na Zari na wala sio kiki kama watu wengi wanavyodai ila amesema kwa sasa hataki kumuongelea Zari kwani ameelekeza nguvu zake kwenye kuitangaza albamu yake iliyotoka siku chache zilizopita.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.