Hali ya Mwanadada Rose Muhando ni Tete
Hali ya mwanadada aliyewahi kuwa muimbaji wa injili maarufu miaka ya nyuma ROSE MUHANDO inasemekana kuwa mbaya na kwamba kwa sasa anasemekana kwamba amekuwa akiishi makazi ambayo hakuna anaejua hata ndugu zake na huku akisemwa kuwa ameuza vitu vyake vya ndani vya thamani na hata watoto wake kukosa malezi na kushindwa kuendelea na shule.
Mwanadada huyo ambae alionekana katika kanisa moja huku jijini anasema kuwa alitwa jukwaani na mchungaji na kupandish ana mapepo huku mkono wake mmoja ukiwa umevunjika na hata sehemu zake za mwili kuonekana zikiwa zimeungua.
Hata hivyo alipokuwa akiombewa alionekana kuongea mambo mengi huku akisemwa kuwa ni mtu aliyefirisika na kwamba hata watoto wake wamekuwa wakiangaika na kukosa kwenda shule kwa kukosa ada.
Rose muhando ni moja ya wasanii waliowahi kutikisa sana katika anga za muziki wa injili na kufanya mambo mengi katika muziki lakini hata alipokuja kuharibikiwa amekuwa chini sana.