Hamisa Amtaka Diamond Aongee na Familia Waache Kumuandama

Hamisa Mobetto alijikuta katika wakati mgumu mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya familia nzima ya Mzazi mwenzake Diamond kumuandama.

Tangu ijulikane kwamba Diamond amerudisha majeshi kwa Hamisa baada ya kumwagwa na Zari, familia yake imeweka wazi kuwa haimkubali Hamisa na hawamtaki.

download latest music    

Lakini juzi mambo yalimfika shingoni Hamisa baada ya Mama Diamond na wifi yake Esma kumpa kichambo cha maana kwa kudai kuwa ni mchafu na hajui hata kusafisha chumba.

Baada ya povu hilo kuendelea kwa muda mrefu huku familia hiyo ikionyesha wazi kabisa kuwa wanamtaka Diamond arudiane na Zari, Hamisa alishindwa kuvumilia.

Hamisa alienda Kwenye ukurasa wa Instagram wa Diamond na kumtolea povu huku akitaka awaambie familia yake waache kumsema kwani wamemsimanga sana:

Hamisa alitoa povu hilo baada ya kuona familia ya Diamond inazidi kumuandama mtandaoni na Diamond haonyeshi jitihada zozote katika kumtetea yeye kama mama watoto wake dhidi ya familia yake mwenyewe.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.