Hamisa-Kuna Msururu Wa Wanaume Wanataka Kunioa

Msanii wa Bongo fleva na mwanamitindo maarufu Hamisa Mobetto amefunguka na kudai Mpaka sasa kuna msururu mkubwa wa wanaume waliopanga foleni kutaka ndoa naye.

Hamisa ambaye alizidi kujizolea umaarufu baada ya kuzaa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amedai ingawa kuna wanaume wengi wanataka kumposa amekuwa akikataa.

download latest music    

Kwenye Interview na kituo kimoja cha habari hivi karibuni Hamisa amefunguka haya kama sababu ya kukataa ndoa na wanaume waliotayari kumposa ni kukosa nao chemistry:

Wapo wengi tu ambao wamekuja kutaka kutoa posa lakini kuoana na mtu mnatakiwa muwe na chemistry moja. Mimi na Diamond tushakuwa na mtoto lakini nina mwingine pia kama alivyo yeye”.

Hamisa amekuwa Kwenye Mahusiano na Diamond kwa miaka zaidi ya kumi lakini hawajawahi kuanika mahusiano hayo hadharani kabisa mpaka leo hii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.