Hamisa Mobetto Aanika Mipango Yake Ya Kuzaa Tena

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto amefunguka kuhusu mipango ya kuongeza mtoto wa tatu.

Hamisa amefunguka kuhusu suala hilo baada ya tetesi kusambaa kuwa hivi sasa ana ujauzito mwingine wa Diamond.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Wasafi Tv hivi karibuni Hamisa amejibu kuwa hivi sasa anaelekeza juhudi zake kwa watoto wake wawili ambao ni wadogo wanaohitaji kulelewa lakini labda hapo baadae ataongeza.

Kwa sababu watoto wangu bado wadogo sana na sina uhakika kama nataka kuongeza familia au la!, may be in the future hatuwezi kujua future inakuwa vipi au Mungu kapanga huku mbeleni lakini ni jambo la kheri sana“.

Tangu Hamisa arudiane na Diamond Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa hivi sasa ana ujauzito mwingine unaosemekana kuwa una miezi mitano ingawa mwenyewe hajathibitisha hilo.

Hamisa tayari ana watoto wawili mtoto wa kwanza na Majizzo na mtoto wa pili na Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.