Hamisa Mobetto Afunguka Mazito Juu Ya Familia Ya Diamond

Mwanamitindo na Msanii wa muzik wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake ya ‘Madam Hero’ Hamisa Mobetto ambaye pia ni mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz amefunguka mazito juu ya Familia hiyo.

Hamisa ambaye amekuwa hana maelewano mazuri na familia ya Diamond kwa muda mrefu sasa hasa baada ya kuachana na Diamond wiki chache zilizopita ameongea mazito juu ya familia hiyo.

download latest music    

Kwenye Interview aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Hamisa amedai kwamba Mama Diamond alimpigia simu akimtaka arudiane na mtoto wake mara baada ya kuachana naye.

Mama Diamond alinipigia simu nirudiane na Diamond, lakini mawifi ndio hivyo tena”.

Lakini pia Hamisa ameongelea sakata la kumblock Diamond Kwenye akaunti ya mtoto wao Dylan:

Diamond hajielewi, nimem-block insta ya mtoto kwa sababu anashindwa hata kujisitiri, hadi anamuhusisha mtoto kwenye mambo yake, nakosa deal kibao za mtoto kisa mambo yake”.

Hamisa amekiri kuwa ni sauti yake iliyosikika na kusemekana kuwa alikuwa anaongea na mganga lakini amesisitiza kuwa yule Kwenye simu hakuwa mganga bali alikuwa ni shekhe:

Sauti ilikuwa ya kwangu, hakuwa ni mganga alikuwa ni Sheikh kwaajili ya dua, ni vitu vya kawaida sana lakini walirekodi”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.