Hamisa Mobetto Ajibu Tuhuma Za Kuazima Nguo

Mwanamitindo na Muigizaji wa Bongo movie Hamisa Mobetto amejibu tuhuma alizotupiwa wiki iliyopita kuwa ameazima nguo za mtu na kudanganya za kwake.

Sakata hilo lilianza wik iliyopita baada ya Mobetto kuposti nguo aliyovaa Sarah mpenzi wa Harmonize na kusema imetoka kwake jambo ambalo sio la kweli kwani nguo hiyo iliyengenezwa na mwanadada mwingine anayejiita Ab Desgners ambaye alimwandikia ujumbe mwanamitindo huyo kuwa awe mkweli.

download latest music    

Baada ya maneno kuzuka Gazeti la Ijumaa Wikienda lilimsaka mwanadada anayeitwa Aliyah ambaye alidai ndio mmiliki halali ambaye alifunguka:

Ni kweli nguo ni zangu kwani Mobeto alikuja kwangu na kunieleza kuwa anataka achukue nguo zangu avae alafu atasema zimetoka kwake ili anitangazie biashara, na kusema kwamba akipata wateja aniletee, mimi nilikataa, nikasema kama anachukua nguo anitangazie kwa jina langu la sivyo nimuazime tu arudishe”.

Baada ya Tuhuma hizo Hamisa alifunguka  na kudai kuwa habari hizo ni za uongo na kilichotokea ni kutoelewana tu:

Jamani mimi nilishaeleza sana na hata nilipoweka kwenye mitandao niliandika kuwa nguo hizo zimebuniwa na yeye sasa mimi nashangaa watu wananichafua kwenye mitandao“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.