Hamisa Mobetto Akiri Kulimiss Penzi la Diamond

Mwanamitindo na msanii wa Bongo movie, Hamisa Mobetto amekiri kulikumbuka penzi la mzazi mwenzake ambaye ni staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Hamisa na Diamond walikiri kuwa na mahusiano ya siri kwa miaka tisa mpaka yalipomwagwa wazi mapema mwaka jana walipozaa pamoja mtoto wao wa kiume anayeitwa Dully au Dylan.

download latest music    

Baada ya mahusiano yao kuwa hadharani wawili hao waligeuka maadui kwenye mitandao ya kijamii kwani Hamisa aliingia kwenye migogoro kadhaa na mpenzi wa Diamond na mzazi mwenzake Zari.

Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kuhusiana na mahusiano yake Hamisa amewashangaza wengi siku chache zilizopita baada ya kuandika ujumbe ulioashiria kabisa umemlenga mpenzi wake wa zamani Diamond.

Ambapo kupitia ukurasa wake wa Snapchat, Hamisa maneno yalioashiria yeye kumkumbuka mpenzi wake wa zamani:

Sometimes i miss you but my heart no longer hurts like it used to, I miss you but I don’t want you back..sijui nimwamini nani kwenye safari ya penzi  langu nimkabidhi usukani akawe dereva wangu maana majanga nalilia kisicho changu..kwenye nyumba ya kupanga nadai kodi wenzangu”.

Baada ya kuandika ujumbe huo watu wengi walimjia juu kwa kutangaza amemiss Diamond wakati anajua fika ana familia na mwenyewe kwa maneno yake amekiri kuwa analilia kisicho chake.

Hamisa alipotafutwa na chanzo kimoja cha habari kuhakikisha endapo ujumbe huo umemlenga Diamond hakupatikana lakini mama mzazi wa Hmisa anayejulikana kama Mama Mobetto alifunguka yafuatayo kuhusiana na mwanaye kumkumbuka Diamond:

Jamani sisi mambo hayo kwenye mitandao mda huu hatuna tena hata mwanangu ameshayasahau hayo mambo badala yake yupo bize na mambo yake mengine..michakato yetu sisi ni kutafuta pesa na si mengine na wala hatutaki kumsikia huyo Diamond”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.