Hamisa Mobetto Akiri Kuwa Katika Kipindi Kigumu

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Hamisa Mobetto ameanika undani juu ya mambo anayopitia kwa hivi sasa na kukiri kuwa katika kipindi kigumu.

Hamisa amekuwa Kwenye headlines tangu alipotangaza kuzaa mtoto wa Diamond mwaka jana lakini siku chache hizi mambo yamekuwa mazito kidogo kwa upande wake.

download latest music    

Familia nzima ya Diamond kuanzia mama yake mpaka Dada zake mpaka mameneja wa Diamond wameonekana kumkataa kata kata Hamisa huku wakionyesha wazi kumpenda zaidi Ex wa Diamond Zari.

Hamisa amekuwa akirushiwa vijembe na Familia ya Diamond ambayo imedai kuwa ni mchafu na hata kusambaa kwa Tetesi kuwa amechezea kipigo cha mbwa koko kutoka kwa Mama Diamond.

Kupitia ukurasa wake wa Snapchat Hamisa amefunguka magumu hayo anayopitia kwa hivi sasa ambapo amesema licha ya magumu anayokabiliana nayo kwa sasa bado anaamini Mwenyenzi Mungu atamvusha:

Bado sijafika Mw/Mungu aliponipangia na kama mnavyoona barabara yangu ni mbovu, ina mashimo, mabonde na pia matope mengi kwa hiyo safari yangu inakuwa ngumu kidogo.

Lakini naimani sana na M/Mungu alonileta kwenye dunia hii, naimani ipo siku nitafika na Naimani barabara yangu hii nii mbovu ipo siku ataisawazisha na kuiweka rasmi.

Nina kushukuru sana Mungu, naimani kuna vibaya vingi umeniepusha navyo na pia naimani kuna vikubwa vizuri vyaja. Na naimani hivi vyote visingenipata mimi kama ningekuwa sina u-special wowote ndani yangu”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.