Hamisa Mobetto Alamba Shavu La Milioni 60 Kupitia Ubalozi

Msanii wa Bongo movie na Mwanamitindo maarufu Hamisa Mobetto amelamba shavi Nono baada ya kuteuliwa kuwa balozi wa Prima hair.

Global Publishers wanaripoti kuwa Hamisa Mobetto  analipwa shilingi milioni 5.7 kwa mwezi (zaidi ya milioni 60 kwa mwaka) leo Agosti 8, 2018, baada ya kuingia mkataba wa mwaka mmoja wa kuwa balozi wa kiwanda kinachotengeneza nywele (rasta) cha Prima Afro, kilichopo Tabata, Matumbi jijini Dar.

download latest music    

Hamisa Mobetto alitangaza habari hiyo njema Kupitia mkutano wake aliofanya na waandishi wa habari ambapo aliweka wazi kuwa kampuni hiyo walikuwa wakimchunguza  nguvu yake kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya kunichunguza, walinifuata ofisini kwangu tukazungumza, nikausoma mkataba na kuangalia masharti yao na kiwango wanachotaka kunilipa niliporidhia tukapanga siku ambayo ni leo nikasaini”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.