Hamisa Mobetto Atoa Baraka Zote Ndoa Ya Lulu na Majizzo

Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto ameweka wazi kuwa hana kinyongo na kutoa baraka zote kwa ajili ya ndoa ya Lulu na Majizzo.

Hamisa amewahi kuwa kwenye Mahusiano na Majizzo siku za nyuma na  kuzaaa naye mtoto mmoja ameweka wazi kuwa hivi sasa hana matatizo na Majizzo wala Lulu hivyo kwake ni Poa tu wakifunga ndoa.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Mobeto alisema kuwa hana kinyongo na Lulu kama ambavyo watu wanasema kwa kuwa mapenzi yake na Majizzo yalishakwisha siku nyingi.

Mimi na huyo anayetaka kumuoa tulishamalizana, hivyo hakuna tena hata chembe ya mapenzi zaidi ya uhusiano wetu wa kulea mtoto.

Kwa maana hiyo sina shida kusikia Lulu anaolewa na siku ya sherehe nikipewa kadi nitakwenda“.

Tangu Lulu atoke jela Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa yeye pamoja na mpenzi wake Majizzo wanategemea kufunga ndoa hivi karibuni na taarifa hiyo ilithibitishwa na Mkuu wa Mkoa Paul Makonda.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.