Hamisa Mobetto Atoa Neno Kwa Wote Wanamuonea Wivu

Muigizaji wa Bongo movie Hamisa Mobetto ambaye pia ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, ametoa neno kwa watu wote wanaomuonea wivu.

Hamisa amekuwa Kwenye headlines kwa muda mrefu sana na wiki hizi chache ameonekana kupitia katika kipindi kigumu na Familia ya Diamond kumkana hadharani.

download latest music    

Hamisa aliweka wazi kuimizwa na vitendo vilivyokuwa vinafanywa na Familia ya Diamond ambayo ilionyesha wazi kuwa haimtaki na kumtaka Diamond kurudiana na Zari.

Lakini sasa Hamisa anaonyesha kuwa hatakaa chini na kusema semwa ovyo kwani amewapa ujumbe mzito wale watu wote wanamuonea wivu Kwenye maisha yake na hata maendelea yake:

Kama unakasirika, unahuzunika au unaona wivu pale mtu anapofanikiwa, Tafadhali inamisha kichwa chako chini, funga macho yako na kisha unyanyue mikono kisha sema “Mungu mimi ni mchawi niokoe”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.