Hamisa Mobetto Awachana Wasiopenda Penzi Lake na Diamond

Muigizaji wa Bongo movie na video vixen maarufu Hamisa Mobetto amewachana watu wote wasiopenda Mahusiano Yake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Hamisa na Diamond wamerudiana penzi lao rasmi na inaonekana wazi kabisa hivi sasa mambo ni moto kwani Diamond ameonekana ana ukaribu sana na mtoto wao Dylan tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma.

download latest music    

Lakini tangu wamerudiana Kumekuwa na maneno mengi yanayosemwa ikiwemo na Mama Diamond kumkataa Hamisa na hata baadhi ya mashabiki kumtolea maneno ya kejeli Hamisa na Diamond.

Hamisa amewapa za Uso watu wote wasiopenda Mahusiano yao ambapo Kwenye mahojiano na Dizzim Online, Hamisa amesema maneno hayawssumbui kwani ndio wapo wote hivyo:

Unajua huwezi kumlazimisha mtu apende pilau wakati alishazoea biriani kwaiyo ni hivyo ni maisha yangu na ni maisha ya watu wengine kwaiyo utakachoona wewe kinakufaa haimaanishi na mimi kitanifaa kwaiyo kila mtu aangalie maisha yake waniache na mimi na maisha yangu.

Mimi sio mtu wa kumridhisha kila mtu maana mimi sio Mungu kwaiyo kama hutaki acha sio lazima what you see is what you get and what you don’t see is what you don’t get”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.