Hamisa Mobetto Azidi ‘Kuwaka’, Angalia Picha Zilizoibua Tetesi za Hamisa na Diamond Kurudiana

Mwanamitindo, muigizaji wa Bongo movie na mzazi mwenza wa msanii Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto amezidi kukamata headlines huko kwenye mitandao ya kijamii.

Hamisa amezidi kupendeza na kuwa mcharo wa hali ya juu hii inatokana na kuanza kupata kazi ndani na nje ya nchi ambazo zinamuingizia kipato fulani na inaonekana kabisa maisha yake yamebadilika.

download latest music    

Baada ya tetesi kusambaa kuwa Hamisa ameshinda kesi yake mahakamani dhidi ya Diamond wiki iliyopita ambapo inadaiwa kuwa mahakama ilimuamuru Diamond kutoa pesa ya matumizi kwa ajili ya malezi ya mtoto wao.

Baada ya kesi hiyo kuisha na Diamond kuthibitisha kuwa wamepatanishwa na hivi sasa hawana ugomvi wowote, tetesi zilianza kutembea kuwa Hamisa na Diamond wamerudiana ndio maaana wamemaliza zile tofauti zao mahakamani fastaa na ndio maana Diamond kakubali kutoa pesa kirahisi.

Siku ya jana tetesi za Hamisa kurudiana na Diamond zilizopita kupamba moto mtandaoni baada ya kusambaa kwa picha na video zilizomuonyesha mpiga picha wa Diamond anayeitwa Lukamba ambaye amekuwa ni mpiga picha ambaye ana mpiga picha Diamond na timu nzima ya Wasafi lakini pia amekuwa akimpiga picha Zari na hata akienda South Africa amekuwa akifikia nyumbani kwa Zari.

 

Hiyo picha hapo juu inamuonesha photographer Lukamba ambaye ni mpiga picha wa Diamond akiwa na Hamisa huku tetesi zikisambaa kuwa alitumwa na Diamond akampige picha lakini Lukamba kwa chini akiwa kwenye picha ya pamoja na Zari.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.