Hamisa Mobetto Hana Kipingamizi Cha Ndoa na Diamond

Mwanamitindo na mfanyabiashara Hamisa Mobetto amefungukia mipango ya ndoa na Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na kuweka wazi kuwa Yupo Tayari Kuolewa naye.

Kwenye mahojiano na Gazeti la Amani, Mobetto alipoulizwa kuhusu utayari wa kufunga ndoa  na Diamond alikubali na kusema Yupo Tayari kufunga naye ndoa:

download latest music    

NDIYO NITAKUBALI, Ingawa Wapo wanaume wengi tu ambao wamekuja kutaka kutoa posa lakini kuoana na mtu mnatakiwa muwe na ‘chemistry’ moja, mimi na Diamond tushakuwa na mtoto, lakini nina mwingine pia kama alivyo yeye”.

Lakini pia Mobetto aliulizwa kuhusu maovu yote ambayo Diamond amekuwa akionekana akifanya na wanawake mbali mbali na Hamisa alifunguka:

Makosa yapo lakini hayo naweza kuyaangalia mbele lakini siyo kwa sasa, kama ni mtu mwenye nia njema na mimi ataonekana”.

Diamond ambaye amewahi kukiri kuwa Kwenye Mahusiano na Hamisa kwa zaidi ya miaka 10 kwa siri, amesemekana kuwa Kwenye Mahusiano na Hamisa tangu alipoachana na Zari mapema mwaka huu.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.