Hamisa Mobetto: Najua Watu Wataniona Mnafki Lakini Nampenda Lulu

Mwanamitindo na mzazi mwenza wa Mwanamuziki Diamond, Hamisa Mobetto amefunguka tena kuhusu kesi ya Lulu Michael na kudai kuwa anampenda sana Lulu ingawa anajua watu wengi watamuona kama mnafki.

Lulu na Hamisa siku zote wamesemekana kuwa maadui kutokana na Lulu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Majizzo ambaye ni baba wa mtoto wa kwanza wa Hamisa aitwaye Fantasy. Habari za chini ya kapeti zinadai kuwa hapo zamani Hamisa na Lulu walikuwa marafiki lakini urafiki huo uliingia doa na kugeuka maadui baada ya Hamisa kuachana na Majizzo kisha Lulu kuanza kutembea naye.

download latest music    

Lakini juzi baada ya kifungo cha Lulu, Hamisa alimuandikia Lulu ujumbe huku akidai kuwa atamiss. Kwenye mahojiano aliyofanya na Clouds Tv, Hamisa amedai kuwa pamoja na hayo yote bado anampenda Lulu:

Namjua Lulu and then namjua Mama Kanumba na upande wa Kanumba, miaka miwili nyuma mimi na Lulu tulikuwa na ugomvi ambao kila mtu anajua sababu sio lazima niongee hapa lakini linapotokea jambo kama hili lililomkuta Lulu  ambalo sio zuri ukaongea kitu fulani wapo watakaochukulia kwa nia mbaya au wakakuona mnafki ila kwangu mimi sina naye tatizo naweza sema kuwa nampenda hasa amekuwa mtu mzuri kwa mwanangu yaani Fantansy ukimuonesha tu picha ya Lulu anafurahi anajua ni anti yake”.

Baada ya Hamisa kuandika ujumbe wa kumlilia Lulu alipofungwa miaka miwili watu wengi waliibuka na kumuita mnafki kwa kile walichodai kuwa Hamisa amesubiri mpaka Lulu amefungwa ndo kusema hawana ugomvi.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.