Hamisa Mobetto Ndani Ya Bifu Zito na Familia Ya Diamond

Mzazi mwenza na mpenzi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto amejikuta katika kiti cha moto baada ya familia ya Diamond kumgeuka na kumuwashia moto kwenye mitandao ya kijamii.

Sakata hili lilianza siku ya Ijumaa baada ya  Diamond kuachia wimbo na video yake mpya ya wimbo unaoitwa Iyena aliomshirikisha Rayvanny ambapo ndani ya wimbo huo Video Queen ni Zari.

download latest music    

Sio siri kuwa Hamisa pamoja na kwamba amerudiana na Diamond lakini hana uhusiano mzuri na familia ya Diamond ambayo ilishaweka wazi kuwa hainpendi na haimaanishi kwani ni juzi tu kulikuwa na sakata kati ya Hamisa na Mama Diamond.

Baada ya wimbo huo wa Iyena kutoka mara moja ya Mama Diamond alianza kuposti wimbo huo na vijembe juu kwa hamisa na kudai kuwa ni mchafu hajui hata kutandika kitanda huku akimsifia Zari na alionyesha wazi kuwa anataka mwanaye arudiane na Zari.

Hata Dada wa Diamond, Esma alimtolea povu Hamisa na kuweka wazi kabisa kuwa amemiss Zari na kuandika ujumbe huu:

Familia ya Diamond ilionyesha wazi kuwa hamtaki Hamisa huku ikidaiwa chanzo cha kumchukia ni baada ya Hamisa kuwaitia Shilawadu siku walioenda hospitali kumuangalia alipokuwa amejifungua.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.