Hamisa Mobetto: Nimefurahia Maamuzi ya Mahakama

Siku ya jana supastaa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na mzazi mwenzake mwanamitindo Hamisa Mobetto walifika tena mahakama ya Kisutu kwa ajili ya muendelezo wa kesi iliyofunguliwa iliyofunguliwa na Hamisa dhidi ya Diamond.

Walifika mahakamani hapo kwa ajili ya kuweka rekodi ili mahakama na ustawi wa jamii waweze iwe na kumbukumbu ya usuluhishi wao mara ya mwisho na ahadi zao walizowekeana.

download latest music    

Baada ya kutoka mahakamani msanii Diamond alifunguka na kuongea na waandishi wa habari na alifunguka yafuatayo:

Labda tu cha kuzungumza kama nilivyosema mara ya mwisho tuliitwa kwa ajili ya usuluhishi na wala sio kesi ilikuwa tunaangalia ni kwa namna gani tutamlea mtoto vizuri tukalifanya hilo likakaa sawa kwaiyo leo tulikuwa tunaweka rekodi ili hapa ustawi na mahakama wawe na kumbukumbu sahihi ili kesho na keshokutwa kisije kikazungumzwa kitu kingine cha uongo lakini mwisho wa siku tumlee mtoto wetu akue maana anaweza akaja akawa kiongozi mkubwa hapa nchini”.

Lakini pia Hamisa aliongea na Millard Ayo Tv ambapo aligunguka na kusema amefurahishwa na maamuzi ya mahakama:

Kwa kweli maamuzi ya mahakama nimeyafurahia kwa sababu ni maamuzi ambayo pande zote mbili tulijadiliana na tukakibaliana nayo nashukuru tu kila mtu ameridhika na maamuzi hayo na yamekwisha”.

Baada ya kumaliza kesi hii Diamond na Hamisa wamekiri kumaliza maneno yao ya mitandaoni na kujikita katika kumlea mtoto wao, Tuwatakie kila la kheri.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.