Hamisa na Zamaradi Ndani Ya Bifu Zito

Mtangazaji na mfanyabiashara Zamaradi Mketema ameingia ndani ya bifu zito na Mzazi mwenza wa Diamond Platnumz Hamisa Mobetto wameingia kwenye majibizano makali Kwenye mitandao ya kijamii.

Kisa cha majibizano hayo ni baada ya kuwepo kwa tuhuma za Zamaradi kuiba idea ya mshono wa nguo yake aliyovaa Kwenye 40 ya mtoto wake kutoka kwa Hamisa Mobetto kisha kwenda kushona kwa fundi mwingine bila hata taarifa.

download latest music    

Baada ya tetesi hizo Zamaradi aliandika Kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa hakuchukua idea ya mshono kutoka kwa Hamisa  bali yeye ndiye alimpa Hamisa mshono lakini alishindwa kushona kwake kutokana na muda.

Nimeambiwa nilipewa mshono na mtu nikaenda kushona kwingine, na nimeshangazwa na uongo mkubwa wa namna hii, Mimi ndio nimetuma mshono kwake na sio yeye, hakuwa anaufahamu kabla, kutokana na kudai kupishana na muda nikaamua nikashone kwingine na zaidi swala la kushona kokote ni uamuzi wangu since sijachukua mshono wa mtu”.

Baada ya povu hilo la Zamaradi, Hamisa na yeye alimwaga povu zito sana na kuandika haya kupitia ukurasa wake wa Instagram:

https://www.instagram.com/p/BmdYoQZlCv_/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1as2jxfy2tqvq

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.