Harmonize adai kuwa ‘kuna mtoto na kuna mtoto wa kizungu

Harmonize kwa hivi sasa ameweka wazi anatoka na mtoto wa kizungu na kama mwanaume yeyote ambaye amelowa kwenye mapenzi, msanii huyu hajakuwa akificha furaha yake.

download latest music    

Msanii huyo wa Wasafi records alimzindua mrembo huyo hivi karibuni baada ya kuwachana na Wolper ambaye alikuwa mpenzi wake kwa muda mrefu. Hata hivyo akiongea kwenye kipindi cha 255 ya XXL ya Clouds FM Harmonize alisisitiza kuwa anatarajia mtoto wake atachukua rangi ya mamake.

Alisema,

“Ngoja nikwambie kitu kuna kuzaa mtoto na kuna kuzaa mtoto wa kizungu ni vitu viwili tofauti,” alisema Harmonize. “Naenda Marekani mara moja si unajua mke wangu anatakiwa kusarifi kaniambia kuna ishu tunaenda kufanya sasa mimba ikiwa kubwa atazuiliwa kupanda ndege,”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua